100/recent/ticker-posts
KANAANI MPYA - Lisikilizeni Neno la Bwana............. MAOMBI NA MAOMBEZI --- Tupigie; +255767-155-623 Ujumbe mfupi/Whatsapp; +255620-179-783

KAZI YA TOBA

KAZI YA TOBA

 

•    Inatupa uhalali wa kuelewana na Mungu.
•    Inatupa uhalali wa kumshughulikia shetani ipasavyo.
•    Inamwondolea haki shetani na kutuweka sisi katika nafasi nzuri ya ushindi.
•    Inatuwezesha sisi kuweka na kuanzisha mawasiliano mazuri na Roho Mtakatifu.
•    Hutuingiza katika neema ya Mungu
•    Humpa Mungu kibali au nafasi kuanza kufanya kazi na sisi.
•    Toba ikikamilika inaleta utimilifu wa utii wako. Isaya 57:15

•    Baada ya kuomba Mungu anayajua yaliyotendeka kwenye mila zetu.
•    Chukua jambo moja moja na kiri mbele za Mungu katika uovu uliofanywa na babu zetu.
•    Walawi 26:40-42.
•    Ebrania 7:9-10 Tulishiriki yale ambayo Babu zetu walifanya
•    Damu ya Yesu ni malipo makamilifu yaliyofanyika
Ebrania 9:11-15
•    Nenda kwa Imani na kuipeleka Damu ya Yesu
•    Kitu ambacho kitakutoa hapo ni maombi.
Ebrania 12:22-24 Damu ya Yesu inanena hata leo.
Hesabu 35:33 Damu ya kulipwa kwa Damu.
•    Kanusha, simama katika mambo ambayo Yesu aliyafanya pale Msalabani Kol: 2:14.
•    Kila jambo ambalo lilikuwa linafanyika katika maisha yetu shetani alikuwa anaandika.
Aliandika katika anga, nyota, mwezi, jua na ardhi.
•    MWanzo 1:26 Mungu alimkusudia mwanadamu atawale bahari na vitu vyote pia.
•    Zaburi 19:1 Amka mapema asubuhi utangaze ukuu wa Mungu.
•    Kanusha na kataa makubaliano yaliyofanywa na mababu zetu
•    Yer:10-11 Mwambie wewe sio Mungu wewe ni pepo.
•    Usiwe na haraka kwenye Madhabahu ya Bwana. Hii ni vita kiroho penye Madhabahu ya Bwana.
•    Kama akishindwa kuchukua dhabihu kwenye Madhabahu ya Bwana, atakuja kwako kukuchafua wewe. Anajua huwezi tena kusimama kwenye Madhabahu.
•    Anataka uchafuke usitoe kitu chochote kichafu katika Madhabahu ya Bwana.
•    Kutoka 20:24 Madhabahu inayojengwa kwaajili ya Mungu, Mungu anakuja kukubarikia.
•    Mahali ambapo panafaa kujenga Madhabahu ni mahali ambapo Mungu mwenyewe amepachagua.
•    Mwanzo 22:1-14 Mahali ambapo Mungu amepachagua akutane na wewe ni mahali ambapo Mungu anapaangalia.
•    Unapofika mahali pa kuabudia hutakiwa kumshirikisha mtu mwingine (au mahali pa matengenezo).
•    Ibrahimu hakumshirikisha Sara alipokuwa anakwenda kumtoa Isaka Sadaka.
•    Kuna mambo mengine Mungu anasema na wewe binafsi si vizuri kumshirikisha mtu mwingine. Unapoenda kwenye Madhabahu ya Mungu Yehova kuabudu unakwenda wewe mwenyewe binafsi
•    Lazima uwe makini unapoenda kumshurikisha mtu shida zako, kila mtu ana Mungu wake.
Amosi 5:21:27 Mungu anachukia makutano yenu na nyimbo zenu.
•    Ndani yao walikuwa na miungu mingine, waliokuwa wakiiabudu.
•    Hata sadaka yao haiwezi kuleta matunda kama kuna Mungu mwingine ndani yake.
•    Mungu alimkatalia Daudi asimjengee nyumba kwasababu mikono yake ilimwaga damu. Ndani ya Hekalu kuna Madhabahu.
•    Isaya 61:1 Mwanadamu ndio hekalu la Mungu.
•    1Kor. 3:16-17 Na roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ndani ya mtu imo madhabahu ya Mungu.
•    Mwanadamu kabla hajaokoka ndani yake shetani alishapanda kitu ndani yake mwanadamu.
•    Kabla ya kuvunja hiyo Madhabahu mwanadamu hawezi kushinda dhambi, hasira, chuki n.k.
•    Watu wengi wamefungwa na uongo n.k
•    Katika hili huwezi kusonga mbele katika mambo ya Mungu
Isaya 52:2-6 Mungu anasema jikung’ute mavumbi kazi ya kujenga Madhabahu ni yako mwenyewe sio Mungu.
Amuzi 6:16-32 Gideoni anamjengea Mungu Madhabahu.
•    Mungu anamwambia aende kwanza akabomoe Madhabahu ambayo baba yake aliijenga
•    Ukitaka kumjengea Mungu Madhabahu ni lazima kwanza ubomoe Madhabahu ambayo ipo. Mstari 26 Ukamjengee Mungu Madhabahu kwa taratibu zake.
•    Mungu anataka umjengee yeye madhabahu mahali anapotaka yeye.
Amosi 10:10-16 Ili Mungu huyu adhihirike itakupasa uiondoe Miungu mingine.
2Falme 10:17-27
•    Mjengee Mungu madhabahu 1Falme 18:30-40 Elia amemjengea Mungu madhabahu.

Post a Comment

0 Comments