100/recent/ticker-posts
KANAANI MPYA - Lisikilizeni Neno la Bwana............. MAOMBI NA MAOMBEZI --- Tupigie; +255767-155-623 Ujumbe mfupi/Whatsapp; +255620-179-783

NGUVU YA IMANI

SOMO: NGUVU YA IMANI


 



 

 

WAEBRANIA 11:1                                                                     

 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo,ni bayana ya mambo yasiyoonekana”




WARUMI 1:17
“kwa maana haki ya mungu inadhihilishwa ndani yake toka imani hata imani kama ilivyo andikwa mwenye haki  ataishi kwa imani.”


IMANI KATIKA KRISTO
v  IMANI ni mwitikio chanya wa roho yako ikubaliane pasipo shaka kuhusu neno la Mungu linavyosema kuhusu wewe na mazingira yanayokuzunguka.
v  IMANI ni mwitikio chanya wa kimatendo mema yanayochochewa na kweli ya neno la Mungu.
v  Kutokana nawaebrania 11:1maana yake imani zaidi ya kile unachokiona katika ulimwengu wa mwili.
Zaidi sana imani ni kuweka moyo wako,macho yako,mdomo wako na vitendo vyako view ndani ya neno la kristo.
·         IMANI siyo hisia
·         IMANI siyo kujitutumua
·         IMANI siyo kupata ulichokuwa unatafuta alafu ukakitendea kazi na ukasema  umepata  kwasababu ya IMANI.
·         Mathayo 17:14-20 ukiangalia mistari hii katika biblia yako utagundua kuwa Yesu aliamua kufundisha imani kwa msisitizo mkubwa mno eneo hili;
“nao walipoufikia mkutano , mtu mmoja akamjia, akampigia magoti, akisema, Bwana umrehemu mwanangu kwakuwa ana kifafa na kuteswa vibaya, maana mara nyingi huanguka motoni na mara nyingi majini.nikamleta kwa wanafunzi wako wasiweze  kumponya .
Yesu akajibu akasema,enyi kizazi kisichoamini , kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini?mleteni huku kwangu.
Yesu akamkemea pepo naye akamtoka , Yule kijana akapona tangu saa ile.kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema mbona sisi hatukuweza kumtoa?  Yesu akawaambia kwasababu ya upungufu wa imani yenu, kwa maana amini nawaambia mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu,ondoka hapa uende kule , nao utaondoka , wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.”
Kwa maandiko hayo machache utaona ni kiwango gani cha imani tunatakiwa nacho ili tuwe na nguvu na uwezo ndani yetu wa kutembea na kusimama mahali popote na katika mazingira yoyote kwa nguvu tu ya imani.




KILICHOPO KWENYE IMANI YA NAMNA HII
HABAKUKI 2:4
“tazama roho yake hujivuna haina unyofu ndani yake lakin mwenye haki ataishi kwa imani yake.”

Kuna kanuni ndani yake ambayo inawawezesha watu wenye imani hiii kupata wanachotaka kwaMungu
        I.            Ukiokoka maisha ni imani bila hivyo maana yake sehemu hautaruhusiwa kupenya .
      II.            Ikifeli imani ndani yako , inamaanisha umefeli kila kitu cha kimungu ndani yako.
    III.            Imani siyo kichwa, siyo fikirabali  Imani ni ya moyo.
    IV.            Mungu hasikii lugha za wanadamu bali Mungu husikia na kutazama kiwango cha  imanikilichoko ndani yako kwa kulinganisha na kitu unachohitaji kupata au kupokea kutoka kwa Mungu kwa wakati huo.
      V.            Imani ilimfanya sara apate mtoto uzeeni ( wanasanyansi wakakaa kimya,  maana imani iliwavunjia kanuni za kisayansi  kwa sara)

( MWANZO 18:9-14) “wakamwambia yu wapi sara mkeo? Akasema yumo hemani, akamwambia hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani , na tazama , sara mkeo atapata mwana wa kiume, sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake.
Basi ibrahimu na sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake, kwahiyo sara akacheka moyoni mwake akisema, niwapo mkongwe nitapata furaha na bwana wangu mzee?   Bwana akamwambia iburahimu mbona sara ameckeka akisema  , mimi kweli nitazaa mwana nami ni mzee?
kuna neno  gani lililo gumu la kumsinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia wakati huu huu mwakani na Sara atapata mwana wa kiume.”

KWAHIYO;
    VI.            Imani inaleta mwonekano mpya ( utukufu mwingine)
  VII.            Pasipo IMANI hakuna kupokea.
VIII.            Imani humuweka mtu karibu na Mungu.


WAEFESO 6:16
zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya Yule mwovu.



MFANO WA MAISHA YA IMANI TEGEMEZI KWA WATU (HASARA TU)
MWANZO 19:26
lakini mkewe Ruthu akatazama nyuma yake, akawa nguzo ya chumvi.
ESTA 3:8-12 Hamani aliweka imani yake kwa Mfalme Ausuero badala ya kuweka kwa Mungu (siku zote kutegemea mtu katika maswala ya imani ni sawa na kuvua nguo wakati wa baridi, au ni sawa na kupewa urithi wa kaburi. Ni mfano wa mtu achekaye msibani.
Mtu ataishi kwa imani yake  wala si ya jirani yake kwa kua imani ya jirani inaweza kukusogeza tu ukatoka ulipokua umekwama lakini hauwezi kuishi kwayo.
Pasipo na imani ya kristo ndani yako , kuna hatari ya mauti  kukuzunguka pande zote kwasababu tunaona namna ambavyo hamani hana msaada tena baada ya kuwa ameweka imani yake kwa mfalme na mfalme huyohuyo hayuko upande wake tena.


UBABE WA IMANI
        I.            Imani ikiwepo uwezo unakuja  , unachipuka ,  unatokeza
      II.            Imani na uwezo vikiungana huleta matokeo yafuatayo
a)      Nafasi ya mtu.ESTA 5:1-2
b)      Kiti cha mtu DANIEL 4: 34-37
Nebukadineza alipo jaa imani
Ghafula kutazama kwakwe kukawa juu na fahamu zake zikamrudia na  ufalme wake ukathibitika tena baada ya kufukuzwa miaka saba katika ufalme au kiti chake cha mamlaka.
    III.            Imani isipokuwepo uwezo unapotea kama ifuatavyo
a)      Imani kuyeyuka MWANZO 18:12kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake akasema niwapo mkongwe nitapata furaha na bwana wangu mzee?
b)      Imani ina poromoka MATHAYO 14:28-30Petro akajibu akasema, ikiwa ni wewe  niamurunije kwako juu ya maji,  29 akasema njoo.petro akashuka chomboni  akaenda kwa miguu juu ya maji ili kumwendea Yesu.lakini alipouona upepo akaogopa akaanza kuzama,  akapiga yowe,  akisema bwana niokoe……………
Watu wamekua mashabiki wa mambo ya imani lakini hawaamini chochote, lolote kwa namna hii wamekua na imani yenye monekano wa kininja kuonekana na kupotea .
Nami nataka nikwambie kuwa kama Yesu hasingelimsaidia Petro,Petro angezama na angekufa na imani yake hiyo ndogo,SIKIA namaanisha hivi kuna kiwango cha imani hakitoshi kabisa kukuvusha mahali haijalishi unamtegemea Mungu kiasi gani,sote tunajua kuwa Petro alikuwa mwanafunzi wa Yesu na alikuwa karibu naye wakati mwingi lakini kupitia upungufu wa imani yake , mauti ilikuwa tayari kumbeba lakini asante YESU mwenye huruma alimsaidia wakati akizama,hivyo ndivyo wakristo wengi leo wanaishi katika imani haba na kwakweli kuna mahali wamevuka si kwasababu ya imani yao kubwa bali kwasababu yesu alikuwepo hapo karibu na akawasaidia wasizame au kuanguka.
Huruhusiwi kuchukua chochote kwenye ufalme wa mungu bila kuwa na fail la ushahidi ( na ushahidi ni imani nayo hutokana na neno  la kristo WARUMI 10:17 basi imani chanzo chake nikusikia na kusikia huja kwa neno  la kristo.



AINA  MBILI ZA IMANI

1.       IMANI YA KIMUNGU
Imani hii ni kuu kuliko imani zote ni ya kwanza na ya mwisho japo zipo imani nyingi sana lakini nimeipa nafasi ya kwanza katika somoletu la leo.

MARKO 11:12-24
inatupa picha juu ya aina hii ya imani ya kimungu (………. hata asubui yake walipotoka bethania aliona njaa. Akaona na kwambali mtini wenye majani akaenda ili labda aone kitu juu yake na alipo ufikilia hakuona kitu ila majani,maana si wakati wa tini ,akajibu akauambia tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia………)
msitari wa 19 unaanza kukufunulia kitu tulicho kisoma kwenye mstari wa 14 ilikuonyesha tatizo la wanafunzi wa Yesu kuhusu imani ya kimungu pasingekua na tatizo mstari wa 19 na kuendelea usingekua na maana.

………….na kulipokuwa   jioni alitoka mjini,na asubui walipokua wakipita Waliona ule mtini umenyauka  toka shinani.
Petro akakumbuka habari yake akamwambia Rabi tazama mti ulioulaani umeyeyuka.
 Yesu akajibu akamwambia mwaminini  Mungu.
 Amini nawaambia yeyote atakaye uambia mlima huu ng’oka ukatupwe baharini,wala asione shaka moyoni mwake ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakua yake.
Kwa sababu hiyo nawaambia yeyote myaombayo mkisali aminini ya kwamba mnayapokea nayo yatakua yenu.

 Jambo ni nalotaka tujifunze  hapa ni namna wanafunzi walivyokua na uwezo mzuri wa kusikia kwa kristo katika mstari wa 14 najambo hili lilitosha kuwafanya wawe na imani maana kutokana na ;
WARUMI 10:17 imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa neno  la kristo, sasa wanafunzi walisikia kwa kristo na ikatosha kuwafanya wawe na imani.
 Bado walikua na tatizo la imani unapo soma mstari wa 19-24 MARKO unaona walisikia lakini hawakuamini;

Mfano;
mtu mmoja mwigizaji alipiga kelele kwenye hotel moja akisema ananjaa sana watu wenye nafasi za  kuhudumu  kwenye hoteli hiyo wakapakua  chakula haraka na kwa ukarimu sana wakamkaribisha chakula, chakushangaza akabaki amekitazama chakula tu.
Huku akisema ana njaa,(njaa inaogopa mtu anayekula)
Njaa haiogopi mtu mwenye chakula  alafu hana uwezo wa kula.
Jambo la kuwa na chakula ni jingine na jambo la kula ni jingine japo ni moja .
Ukiwa na imani alafu huiamini ni sawa na muigizaji ambaye anaigiza lakini uhalisia wa maisha yake haufanani na kile anachokiigiza.

MFANO  huu utakusaidia kuelewa , tatizo la wanafunzi na tatizo lako na tatizo la wengine kuhusu imani ya kimungu.
Tazama tena hapa;

MATHAYO 14:28-32
Petro akajibu akasema Bwana ikiwa ni wewe niamuru nije kwako juu ya maji,
Akasema njoo.
petro,akashuka chomboni ,akaenda kwa miguu juu ya maji.
Ili kumwendea Yesu lakini alipouona upepo akaogopa ,akaanza kuzama ,akapiga yowe akisema,Bwana niokoe, Mara Yesu,akanyoosha mkono wake,akamshika akamwambia,ewe mwenye imani haba mbona uliona shaka? Nao walipopanda chomboni upeo ulikoma .


CHANGAMOTO ZA IMANI HII
Pamoja na kuwa na mafanikio makubwa sana ya imani ya  ya kimungu kwa wenye nayo ukabiliwa na changamoto ya watu kutomuelewa japokuwa wanasikia  anachosema na kuona anachofanya,bado hawawezi kuelewa
YOHANA 11:39-44
Yesu akasema, liondoeni jiwe.martha dada yake Yule aliyefariki , akamwambia, Bwana ananuka sasa , maana amekuwa maiti siku nne.Yesu akawaambia , mimi sikukuambia yakwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?. Basi akaliondoa lile jiwe ,  Yesu akainua macho yake juu, akasema, baba, nakushukuru kwakuwa umenisikia.Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuz ote,lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya , ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.Naye akiisha kusema hayo,akalia kwa sauti kuu, Lazaro njoo huku nje.Akatoka nje Yule aliyekufa,amefungwa sanda miguuni na mikononi na uso wake amefungwa leso.naye Yesu akawaambia,mfungueni , mkamwache aende zake.




IMANI YA KITHOMASO
Aina ya pili katika mpangilio wa somo hili , imani hii inapatikana kwa watu wote wenye kuwaza kibinadamu,imani ya namna hii haina uwezo wa kuamini mpaka ione, wakati imani ya kimungu inataka kuamini kabla hujaona.


Nianze na aina ya mawazo ya kibinadamu yanayodhibitisha imani ya kithomaso.
YOHANA 5:2-8
Inatosha kuichukua imani ya kristo na kuiingiza katika mawzo ya kibinadamu,angalia


Yohana 5:2-8
Na huko yerusalem penye mlango wa kondoo pana birika iitwayo kwa kiebrania bethzatha nayo ina matao matano. ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala , vipofu ,viwete nao waliopooza,(wakingoja maji yachemke.kwamaana  kuna wakati ambapo malaika hushuka akaingia katika ile birika akayatibua maji, Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, akapona ugonjwa wake wote uliokuwa umempata.) na hapa palikuwa na mtu ambaye amekuwa hawezi kwa muda wa miaka thelathini na minane.Yesu alipomwona huyu  amelala,  naye akijua yakuwa amekuwa hali hiyo siku nyingi, alimwambia wataka kuwa mzima? Yule mgonjwa akamjibu Bwana ,mimi sina mtu wa kunitia birikani, maji yanapotibuliwa ila ninapokuja mimi mtu mwingine hushuka mbele  yangu.  Yesu akamwambia,simama jitwike godoro lako uende.

Tazama maandiko haya yanavyokutazamisha shida ya imani ya kithomaso,imani ya mpaka uone,
Imani ya namna hii huwa inaongozwa na mawazo ya kibinadamu,msitari wa 7 huu unadhihirisha ni jinsi gani mtu mwenye imani hii anavyotegemea watu katika mahitaji yake na matatizo yake jambo ambalo ni sawa na kuchuja mbu na kumeza ngamia au kujivunia makaburi yaliyopakwa chokaa,nayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri bali ndani ni mifupa ya wafu na uchafu wote.
Imani hii mungu hapendezwi nayo hata kidogo.
kiu yake msalabani ni kuifunua imani yake ya kweli katika maarifa ya kimbingu za kimbingu,tangu natangu,umilele wa umilele na milele.




MADHARA YA IMANIYA KITHOMASO
 Msitari wa 7 unaonyesha laumu la mgonjwa kwa watu  ambao hawakumsaidia pia akaenda mbali akalaumu na wale waliokuwa wanamuwahi kuingia birikani,
haya mawazo ya kibinadamu Yesu akayavunja kwa nguvu ya agano ambaye ni yeye mwenyewe ambapo kwa asili ni mwenyezi,akasema katika msitari wa 8..simama jitwike godoro lako uende

YOHANA 20:26-29
Basi, baada ya siku nane wanafunzi wake walikuwamo  ndani tena na thomaso pamoja nao , Akaja yesu na milango imefungwa akasimama katikati akasema,amani iwe kwenu. kasha akmwambia thomaso leta hapa kidole chako uitazame mikono yangu,ulete na mkono wako  uutie ubavuni mwangu,  wala usiwe asiyeamini bali aaminiye,thomaso akajibu akamwambia , Bwana wangu na Mungu wangu ,
yesu akamwambia, wewe, kwakuwa umeniona umesadiki,wa  heri wale wasioona , wakasadiki.



Msitari huu wa 29 unatosha kukuondoa kwenye imani ya kithomaso ,Mwenyezi anapenda imani inayoonekana kabla ya vitu halisi.
Niliamini kuyaandika haya kabla sijajua nitaandikaje , lini , wapi , na muda gani.

Ø  Ibrahimu  aliamini kupata mtoto kabla ya kuona katika mwili.
Ø  Daniel alimwamini Mungu kabla ya kujua kama samba watamla au la.
Ø  Meshaki ,shedraka na Abednego walimwamini Mungu  kabla hawajajua kama atakuja awe nao kwenye tanuru la moto.
Ø  hatahivyo nilimwamini mungu wakati watu wawili waliponichukua na kuniingiza kwenye chumba cha ndani alafu wakavua nguo zao  zote alafu wakajikata na kiwembe baadhi ya maeneo ya miili yao na wakachukua nguo mpya walizokuwanazo wakajifutia damu iliyowatoka alafu wote kwa pamoja wakaililia miungu yao na kuishirikisha jambo hilo alafu wakanilazimisha nguo hiyo niivae kwa nguvu kisha wakaniacha nitoke kwenye chumba hicho wakidhani wamefanikisha mambo yao,katika neno la bwana wote walishakufa kwa namna tofautitofauti ,wameacha familia zao katika halia ya ukiwa sawa na mathayo 23:37-39
 Ee Yerusalemu,yerusalemu uwauaye manabii na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja kwako watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka.angalieni nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
kwa maana nawambia hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.



AINA NNE ZA IMANI YA KIMUNGU
1.IMANI NDOGO
Hii ni aina ya imani ya kwanza katika mpangilio wa somo hili.
Sifa za imani ndogo ni kuanzisha jambo lakini kushindwa kulimalizia.
Dalili za imani ndogo ni hofu,wasiwasi na mashaka (upungufu wa neno la Mungu rohoni)
Tazama mathayo 8:23-26
Akapanda chomboni wanafunzi wake wakamfuata,kukawa msukosuko mkuu baharini hata chombo kikafunikizwa na mawimbi,naye alikuwa amelala usingizi.
Wanafunzi wake wakamwendea wakamwamsha,wakisema,Bwana tuokoe tunaangamia.
Akawaambia,mbona mmekuwa waoga,enyi wa imani haba?mara akaondoka akazikemea pepo na bahari, kukawa shwari kuu.


JINSI YA KUVUKA KUTOKA KWENYE IMANI NDOGO
*      Ni kuikuza imani yako kwa kuipandisha imani hata imani.
Warumi 10:17 “basi imani chanzo chake ni kusikia,na kusikia huja kwa neno la Kristo.”
Imani ina tabia ya kukua kutokana na kiwango chako cha kuingiza neno  la kristo ndani yako.


2.IMANI KUBWA
Hii ni imani ya pili katika mpangilio wa somo hili
Imani hii ni kubwa na ni wachache wenye uwezo wa kuwa nayo.
Luka 7:2-10
“Na mtumwa wake akida mmoja alikuwa hawezi, karibu na kufa,naye ni mtu aliyempenda sana.
Aliposikia habari za Yesu , alituma wazee wa wayahudi kwake kumwomba aje amponye mtumwa wake.
Nao walipofika kwa Yesu walimsihi sana wakisema,amesitahiri huyu umtendee neno hili .
maana analipenda taifa letu naye alitujengea sinagogi.
Basi yesu akaenda pamoja nao hata alipokuwa si mbali na nyumba yake, Yule akida alituma rafiki kwake, akamwambia Bwana usijisumbue maana mimi sisitahiri wewe uingie chini ya dari yangu.
kwahiyo nilijiona sisitahli mimi mwenyewe kuja kwako , lakini sema neno moja tu na mtumwa wangu atapona.
kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu,nikimwambia huyu nenda uhenda na huyu njoo huja na mtumwa wangu ,fanya hivi  hufanya.
Yesu aliposikia hayo  alimsitaajabia  akaugeukia mkutano uliokuwa ukimfuata akasema,namwaambia hata katika Israel sijaona imani kubwa namna hii.
Na wale waliotumwa waliporudi nyumbani wakamkuta Yule mtumwa ni mzima.”


Imani ya namna hii hutengeneza njia na kupita yenyewe pasipo kukwama.
Imani kubwa hufanya vyote kama unavyotaka, haizuiliwi na vizuizi vya aina yoyote katika  ulimwengu wa mwili .

3.IMANI DHAIFU
Imani ya aina hii huleta tabia ya kusitasita.
Pia huweza kuzuiliwa kwa urahisi na itaridhia (ina maamuzi finyu)
Inatokana na watu ambao hawajifunzi  utauwa kama Timotheo (jizoesheni utauwa)
Alivyoambiwa na Paulo  warumi 4:17-22
“(Kama ilivyoandikwa nimekuweka kuwa baba wa mataifa mengi) , mbele zake yeye aliye mwamini  yaani Mungu mwenye kuwahuisha wafu,ayatajaye  yale yasiyokuwako kana kwamba  wamekuwako.
Naye aliamini kwa kutarajia  yasiyowezakutarajiwa ilia pate kuwa baba wa mataifa mengi kama ilivyonenwa ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
Yeye  asiyekuwa dhaifu wa imani,alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa, 
( akiwa amekwisha kupata umri kama miaka mia) na hali ya kufa ya tumbo lake sara.
Lakini ukiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini bali alitiwa nguvu kwa imani akimtukuza Mungu.
Huku akijua hakika yakuwa Mungu aweza  kufanya yale aliyohaidi , kwahiyo akihesabiwa kwake kuwa ni haki.”

·         Imani dhaifu ni ile ambayo haioni ngambo ya  matatizo kuna ushindi, wala haina uhakika wa kutoka ilipokwama ( ni hatari sana kua na imani dhaifu).
·         Ibrahim pamoja na kuwa na udhifu wa kuzeeka hakuruhusu imani yake kuwa dhaifu.


4.IMANI YENYE NGUVU
*      Imani hii ni ya nne katika mpangilio wa somo hili niya mwisho kwa mtiriko huu wa somo mpaka hapo Mungu atakaponipa kibali tena cha kuendelea na somo hili .

*      Imani hii huja kwa mtu kwa njia ya kuifanyia mazoezi.
*      kuikaza imani hata imani
*      Imani ya namna hii ina tabia ya kufanya mambo ambayo yakisikiwa na watu masikio yanawasha.(mambo makuu,mambo yasiyotegemewa)
*      Imani yenye nguvu  huanzia moyoni kwa nguvu ,hutokeza bila mpinzani, na hugusa mioyo watu.

Warumi 4:20
“Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini,bali alitiwa nguvu kwa imani akimtukuza Mungu.”
Tazama pia katikaMatendo ya mitume 3:1-8
“Basi petro na yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni saa ya kusali saa tisa.
Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu abaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao Mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu.
Mtu huyu  akiwaona petro na yohana wakiingia hekaluni wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka,
Na petro akimkazia macho, pamoja na yohana akasema ,tutazame sisi.
Akawaangalia akitarajia apate kitu kwao,
lakini petro akasema mimi sina fedha wala dhahabu  lakini nilichonacho ndicho nikupacho.kwa jina layesu kristo wa Nazareti,simama uende.
Akamshika mkono  wa kuume akamwinua mara nyayo zake na vifundo vyake vya miguu yake vikatiwa nguvu.
Akaondoka upesi akasiimama akaanza kwenda akaingua ndani ya hekalu pamoja nao,akienda akiruka-ruka na kumsifu Mungu .”


Nilitaka uone imani yenye nguvu inavyoanzia moyoni kwa nguvu na kutokeza bila upinzani na inafanya kazi kubwa kwa matokeo toshelevu.
Mtu mwenye imani ya namna hii ana uwezo wa kutawala kila kitu duniani na kufanya anavyotaka sawa na mapenzi ya Mungu;
§  Angalia Eliya alifunga mvua hisinyeshe miaka  mitatu na nusu.1wafalme 17:1
§  Angalia Musa alipasua bahari ya shamu.Kutoka 14:21-22
§  AngaliaDaudi alimuangusha goriathi. 1samweli 17:45-50
§  Angalia yoshua kwenye ukuta  wa yeriko. Yoshua 6:1-20
§  Angalia Danieli kwa wale simba. Danieli 6:22

Naomba unisikilize nakukumbusha tu;
§  Esta kwa mfalme ahasuero na Mordekai kwaHamani. Esta 5:1-8:17
§  Yesu pale kisimani alipokutana na mwanamke wa samaria. Yohana 4:1-42
§  Ayubu alivyokutana na mgonjwa .Ayubu 42:7-12
§  Medadi na elidadi katika wakati wa musa.Hesabu 11:26
§  Isaka alipochimba kisima akakiita rehobothi. Mwanzo 26:17-22
§  Korinelio alipotoa sadaka. Matendo ya mitume 10:31
§  Yohana alipotupwa katika kisiwa cha patmo.Ufunuo wa Yohana 1:9
§  Mimi binafsi nilipogongwa na magari mawili kwa wakati mmoja.
§  Mtoto aliporuka tumboni mwa elizabethi baada ya kukutana na Mariam.Luka 1:41
§  Wanafunzi wa yesu walipomsubiri roho mtakatifu.Matendo ya mitume 2:1-4
NB mungu huwa anatembea pasipo kujizuia akishaona mtu ana imani yenye nguvu.

JINSI YA KUIFANYA IMANI YAKO IFANYE KAZI
*      Zipo kanuni baadhi nilizokuandikia kwenye somo hili ila sina maana ya kwamba ndo ukomo wa kanuni hizi.Tutaendelea kujifunza kadri Roho mtakatifu atakavyokuwa akizidi kutufundisha katika mwendelezo wa somo hili.
Kabla ya kanuni hizi kuna maandalizi pia ya kufanya Kwa muhusika Kama ifuatavyo;
Waefeso 6:16-18
Zaidi ya yote mkitwaa ngao ya imani ambayo Kwa hiyo mtaweza kuizima mishale ya Yule mwovu.
 Tena ipokeeni chapoe ya wokovu Na upanga wa roho ambao Ni neno la mungu.
Kwa sala zote Na maombi, mkisali kila wakati katika roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote.

1YOHANA 5:4-12
Kwa maana kila kitu kilichozaliwa Na mungu huushinda ulimwengu Na huku ndio kushinda kushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.mwenye kuushinda ulimwengu Ni nani Isipokuwa ni yeye aaminiye kuwa Yesu ni mwana wa Mungu?huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu ,Yesu kristo si katika maji tu bali katika maji na katika damu, naye roho ndiye ashuudiaye kwasababu roho ndiye kweli,
kwa maana wako watatu washuhudiao  mbinguni baba neno na roho mtakatifu  na watatu hawa ni umoja. kisha wako watatu washuhudiao dunia .
Roho wa maji na damu  na watatu hawa hupatana  kwa habari moja. tukiupokea ushuhuda wa wanadamu,ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi,kwa maana ushuhuda wa mungu ndio huu , kwamba ameshuhudia mwanawe.
yeye amwaminiye ,mwana wa Mungu anao ushuhuda ndani yake.asiyemwamini mungu amemfanya kuwa mwogo kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu ameshashuhudia Mwanawe.
Na huo ndio ushuhuda ya kwamba ,Mungu alitupa uzima wa milele,uzima huu umo katika mwanawe,
yeye aliye mwana, ano huo uzima asiye naye mwana wa Mungu hana huo uzima.


Waebrania 11:8-10
Kwa imani ibrahimu alipoitwa aliittika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi,akatoka asijue aendako ,
kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi,kama katika nchi isiyo yake akikaa katika hema pamoja na isaka na yakobo warithi pamoja naye wa ahadi ileile.
 Maana alikuwa akiutazamaia mji wenye misingi ambao wenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.

Mistari hii kwa namna ilivyo inatosha kwa sehemu kukuandaa vizuri katika kuingia kwenye kanuni za imani katika kufanya kazi.
Nimetumia neno SEHEMU , kwasababu najua kuna nafasi ya roho mtakatifu pia kumuandaa mtu kwenda kwenye kuamini.




KANUNI TATU ZA IMANI KUFANYA KAZI

*      Hizi ni baadhi ya kanuni zilizopo kwenye mfululizo wa somo hili japo Mungu atakaponipa kbali cha kuendelea nitafanya hivyo sawa na mapenzi yake.


1.IMANI ILETAYO MATOKEO
v  Ni lazima ianzie moyoni (chanzo kizuri cha maandalizi ya imani yako ni moyoni)
Warumi 10:10-11
Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu,
kwa maana andiko lanena kila amwaminiye hatatahayarika.

Baada ya kuwa na imani ya namna hii tu moyoni ,hapo ndipo ulimwengu wa roho  hukuhesabia haki na ukihesabiwa haki panakuwa na uhalali wa jambo lolote lililokusudiwa kudhihirishwa kwenye ulimwengu wa mwili na pasipo kuzuiliwa.

2.IMANI YA KUKIRI KINYWANI MWAKO
*      Imani ya kukiri kutoka kinywani mwako yale ambayo moyo wako umeamini (moyo na mdomo viende pamoja)
Mdomo ni kiungo muhimu sana katika ulimwengu wa roho
mfano; mchawi hawezi kufanya chochote bila kutamka .

v  Musa alilazimika ayatamke mapigo ya farao kabla hayajadhihirishwa mwilini
mwanzo 1:3-31
 Mistari yote hii utakuta Mungu kasema , mungu  akasema tazama tumeumbwa kwa mfano wake,  kama yeye alisema nasi inatupasa kutamka kwa imani (tazama pia marko 11:23) Yesu anawafundisha wanafunzi wake jinsi imaniinavyotaka mtu aseme anachoamini moyoni ili kitendeke.
 
 
3.KUSIKILIZA NENO  LA  MUNGU
Hii ni kanuni ya mwisho katika somo hili, ili upate la kusema kinywani mwako, ili ukasikilize akishakusikilizisha anayathibitisha au anayafanya yatokee , sisi ni mfano wa mungu kama mwezi ulivyo mfano wa jua.Mwezi unaakisi jua ili upate mwanga wa kutoa .
Mungu hatimizi neno la mtu yeyote bali anatimiza neno lake, wala imani haitokani na neno  la kibinadamu  bali inatokana na neno  la kristo.
kwahiyo uwe na uhakika ukitaka imani yako ifanye kazi muda wote kwa nyakati zote utamke au useme  kinywani mwako neno la Mungu yaani kristo yesu kuhusu kitu unachokitaka kiwepo , kije , kitokee, kiumbike AU kipone.


Unapotaka  kusema chochote kwa imani hakikisha  una neno  la kristo la kutosha ndani yako.
Yohana 1:1-3
Hapo mwanzo kulikuwapo neno, naye neno alikuwako kwa mungu,naye neno alikuwa Mungu.huyo mwanzo alikuwako kwa mungu,vyote vilifanyika kwa huyo ,wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichonyika.

Yupo pia malaika ambaye huwa anasikiliza tunachotamka alafu anayapa nguvu na kuyatimiza tuyanenayo;
Muhubiri 5:5-6
Ni afadhali husiweke nadhiri kuliko kuiwekausiondoe,usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako wala husiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa,kwani Mungu akukasirikiaye sauti yako na kuiharibu kazi ya mikono yako?

Yakobo 3:2
Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi,Mtu asiyejikwaa katika kunena mtu huyo  ni mkamilifu,awezaye kuuzuia na mwili wake wote kamalijamu.

Mithali 18:21
Mauti na uzima huwa katika uweza wa ulimi na wao waupendao watakula matunda yake.

Nilikuwa najaribu kukutazamisha mistari hii ujue madhara ya kutamka pasipo kujua umesema katika imani ya Neno la kristo au umetamka nje ya imani hii.(kutamka huleta matokeo ya imani)

Nashukuru kwa kuwa umechukua muda wako kusoma na kutafakari somo hili,Mungu wangu katika Kristo Yesu akubariki sana .
Naomba maombi yako sasa ili wakati mwingine nije na ujumbe mzuri  utakaoendelea kufanyika nuru na msaada kwetu katika Kristo Yesu.
Ameni


ISAYA 55:11
Ndivyo litakavyokuwa neno langu litokalo katika kinywa changu,halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.
Somo hili tumeliombea vya kutosha ili lifanyike Baraka katika maisha yako na kupitia somo hili Mungu apate kukuvusha mahali ulipokuwa umekwama kiimani na tangu sasa ukaanze kuona nguvu mpya za kiimani zikiongezeka ndani yako na mpenyo ukitokeza juu ya maisha yako.

MUNGU WANGU AKUBARIKI SANA NA AZIDI KUJIFUNUA KWAKO PINDI USOMAPO SOMO HILI




NEEMA NA USHIRIKA WA MUNGU BABA VIKAWE PAMOJA NAWE
Kwa Msaada Ushauri Na Maombezi
Tafadhali Wasiliana Nasi walimu Wa Neno La Mungu;
Mwl: AZORI MICHAEL           +255767 155 623  (PIGA)
NA
Mwl: JOSHUA        +255620 179 783         ( SMS)
                                                                                                    
  “MUNGU WANGU AKUBARIKI NA KUKUTENDEA MEMA”
 

Post a Comment

0 Comments